New Dar es salaamu( 2016-2017)
THE HOUSE OF NEW BRAND
Monday, 1 August 2016
NEW IN ECONOMIC:HAKI MADINI WAENDESHA MDAHALO WA MAENDELEO YA UCHUMI NA UWEKEZAJI KWENYE MADINI SIMANJIRO.
Mkurugenzi wa Shirika la Haki Madini, Amani Mustafa Mhinda akizungumzia juu ya ugatuzi na ugatuaji wa madaraka kwa wadau wa madini ya Tanzanite wa Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, katika mdahalo wa siku mbili wa maendeleo ya uchumi na uwekezaji kwenye madini unaofanyika Mirerani na kuandaliwa na shirika hilo.
Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Albert Msole (katikati), Diwani wa Kata ya Mirerani Yohana Onyango, (kushoto) na Mwenyekiti wa mtaa wa Twiga Anthony Musiba, wakifuatilia mdahalo siku mbili wa wa maendeleo ya uchumi na uwekezaji kwenye madini, juu ya mpango wa uhamasishaji na uwazi katika katika mapato ya madini, gesi asilia na mafuta unaonyika Mji mdogo wa Mirerani na kuandaliwa na shirika la Haki Madini.
Wadau wa madini ya Tanzanite wa Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, wakifuatilia mdahalo wa siku mbili wa maendeleo ya uchumi na uwekezaji kwenye madini uliondaliwa na shirika la Haki Madini.
No comments:
Post a Comment